Asante! Uwasilishaji wako umepokelewa!
Lo! Kuna kitu kilienda vibaya wakati wa kuwasilisha fomu.

Ulinzi

Nimepoteza simu yangu. Ninawezaje kuzima uthibitishaji wa sababu mbili (2FA)?

Tafadhali wasiliana nasi kupitia mazungumzo mubashara mara moja, na tutakusaidia kuzima 2FA kwenye akaunti yako. Unapokuwa na simu mpya, tafadhali wezesha tena 2FA.

Ninawezaje kuwatambua matapeli wanaojifanya ni watu wa msaada kwa wateja wa Deriv kwenye Telegram?

__wf_reserved_inherit
Mfano wa vikundi vinavyoiga Deriv kwenye Telegram

Lengo kuu la tapeli ni kuiba taarifa zako muhimu na fedha zako.

Hapa kuna baadhi ya njia za kubaini watapeli wa msaada wa wateja wa Deriv:
- Watapeli huomba maelezo yako ya kuingia au taarifa nyingine nyeti kupitia Telegram.
- Wanaweka zawadi ambazo zinaweza kuonekana kuwa njema kupita kiasi.
- Wanaomba malipo kupitia njia zisizoweza kufuatiliwa, kwa mfano, kupitia cryptocurrency.
- Wanaomba upakue programu ambayo haipitishwi katika Google Play Store au Apple App Store.
- Wanaomba upakue programu ambayo inaruhusu kifaa chako kudhibitiwa kwa mbali.
- Wanaomba upakue faili zinazohusisha programu za hasara au virusi ambavyo vinaweza kuathiri kifaa chako.

Bila shaka, orodha hii haijakamilika. Kila siku, matapeli wanakuja na mbinu mpya kujaribu kuiba taarifa zako na pesa.

Ninawezaje kuwa salama dhidi ya matapeli kwenye Telegram?

  • Usitoe taarifa za akaunti yako au taarifa zako binafsi kwa mtu yoyote kupitia Telegram.
  • Kama kitu kinaonekana kizuri sana kuwa kweli, usikiamini.
  • Kamwe usipakue apps kupitia Telegram.
  • Kagua file zote kupitia antivirus iliyosasishwa kwanza kabla ya kuzipakua.
  • Tafadhali hakikisha unajiunga na Deriv group sahihi kwenye Telegram.
  • Ikiwa umewasiliana na mtu anayeweza kuwa tapeli au kama una maswali yoyote, wasiliana nasi kupitia mazungumzo mubashara.

Mifano ya jumbe toka kwa matapeli:

__wf_reserved_inherit

Ninawezaje kutambua barua pepe kutoka kwa matapeli wanaojifanya ni watu wa msaada kwa wateja wa Deriv?

Hapa kuna baadhi ya njia za kutambua barua pepe kutoka kwa matapeli:

  • Barua pepe imeandikwa vibaya, ina makosa mengi yakisarufi.
  • Matapeli watakwambia utume taarifa za siri kupitia majukwaa yasiyo salama, kwa mfano, kupitia SMS, WhatsApp, barua pepe, n.k.
  • Wanakwambia ujaze fomu kwenye wavuti isiyosalama bila unganisho la HTTPS (salama).
  • Wanakwambia upakue apps za simu zisizo salama katika mfumo wa APK faili ambazo hazitolewi kwenye Google play store au App Store.
  • Wanakwambia upakuze viambatisho vya faili au programu za upatikanaji wa mbali (kama Teamviewer) kuwapa udhibiti wa mbali wa kifaa chako. Kwa mfano, mtapeli anaweza kuchukua udhibiti na kusanidi ransomware kwenye kifaa chako na kisha kudai nyeki. Iwapo nyeki haitalipwa, unaweza kupoteza ufaccess wa kifaa chako milele.
  • Matapeli mara nyingi hutumia maeneo ya barua pepe ya bure kama @yahoo.com, @gmail.com, au @protonmail.com. Daima soma anuani kamilifu ya barua pepe ya mtuma ili kujua ni nani aliyetuma barua pepe hiyo. Kumbuka: Barua pepe kutoka Deriv zitakuja kila mara kutoka @deriv.com.
Samahani, hatukuweza kupata matokeo yoyote na“
Hali tupu
” ndani yake

Bado unahitaji msaada?

Timu yetu ya Msaada wa Wateja inapatikana 24/7. Tafadhali chagua njia unayopendelea ya mawasiliano. Jifunze zaidi kuhusu Utaratibu wetu wa malalamiko.

Ilani ya kuelekeza kwingine

Unaelekezwa kwenye wavuti ya nje.